Ronaldo ametangazwa kuwa mchezaji bora UEFA 2016/2017
![](https://s3-us-west-2.amazonaws.com/millard-ayo-bucket/wp-content/uploads/2017/08/24202412/Screen-Shot-2017-08-24-at-8.23.31-PM-660x400.png)
Baada ya Shirikisho la soka barani Ulaya UEFA leo Alhamisi ya August 24 2017 mjini Monaco Ufaransa kuchezesha droo ya hatua ya makundi ya UEFA Champions League msimu wa 2017/2018, walitangazwa mshindi wa tuzo ya mchezaji bora wa Ulaya 2016/2017.
Nahodha wa timu ya taifa ya Ureno anayeichezea Real MadridCristiano Ronaldo ametangazwa kuwa mshindi wa tuzo ya mchezaji bora wa Ulaya 2016/2017 kwa kumshinda mpinzani wake mkubwaLionel Messi wa FC Barcelona na golikipa wa Juventus Buffon.
![](https://s3-us-west-2.amazonaws.com/millard-ayo-bucket/wp-content/uploads/2017/08/24202400/Screen-Shot-2017-08-24-at-8.23.14-PM-950x524.png)
Kutoka kushoto ni Messi, Buffon na Ronaldo
Ronaldo kwa msimu wa 2016/2017 ambapo ameshinda pia tuzo ya mshambuliaji bora 2016/2017, alikuwa na msaada mkubwa kwa club yake ya Real Madrid msimu uliyomalizika lakini ameifungia magoli 12 na kutoa assist 6 katika michuano ya UEFA Champions League.
Hakuna maoni: